Tuesday 28 April 2015

HAPPY BIRTHDAY TO ME

NINA KILA SABABU YA KUMSHUKURU MUNGU KWA HATUA  HII KUBWA ALIYONIWEZESHA KUIFIKIA, HAPA NILIPO MIMI NI NEEMA YAKE TU. PAMOJA NA MAGUMU YOTE NILIYOPITIA KATIKA KUUENDEA MWAKA WANGU HUU IKIWEMO NA MARADHI, NASHUKURU KWAMBA SASA NIKO SALAMA NA NINAENDELEA VIZURI. ASANTE MUNGU KWA KUWA UMEKUWA FIMBO YANGU YA KUINUKIA KILA NILIPOANZA KUANGUKA. PIA NTAKUWA NA TABIA MBAYA KAMA SITAISHUKURU FAMILIA YANGU, BABA YANGU MPENZI AMBAYE AMEKUWA EGEMEO LANGU, KAKA ZANGU AMBAO HAWAKUCHOKA KUNIJULIA HALI KILA SIKU NA KUJUA MAENDELEO YANGU. ANDREW NA JACOB, NAWAPENDA SANA NA MUNGU AWATUNZE BABA ZANGU. MZEE MALUGU NA FAMILIA YAKE, SIJUI NIWALIPE NINI. MAMA MALUGU ULIKESHA NA MIMI USIKU KUCHA, ASANTE SANA MAMA. MUNGU AWATUNZE. DADA YANGU KIPENZI DEVOTHA, SINA LA KUSEMA ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA THAMANI ULIYONAYO MOYONI MWANGU. WEWE NI MAMA YANGU NA ITABAKI KUWA HIVYO MPAKA MUNGU ATAKAPOTUTENGANISHA. NAKUPENDA SANA MAMA YANGU. ANNA, KIBIBI, BUGUMBA, SIJUI NIKUITE JINA GANI MDOGO WANGU. ULIKUWA MKUBWA KWANGU KWENYE HIKI KIPINDI CHOTE MAMA. NAKUSHUKURU KWA KILA KITU, KWANI WEWE NDIO KILA KITU KWANGU NA NDIO MAISHA YANGU. MUNGU AWATUNZE MAANA WEWE NA DADA MLIPIGANA KIUME. KATIKA WOTE SIWEZI KUMSAHAU BEST FRIEND WANGU, RAFIKI YANGU, KIPENZI CHANGU, MUME WANGU, BEGA LANGU LA KULIA,USINGIZI WANGU, RAFIKI YANGU WA KARIBU GODFREY(STEVE). WEWE NDIYE ULIKUWA FARAJA YANGU YA KWANZA, NAHISI BILA WEWE SIJUI INGEKUWAJE BABA. ASANTE SANA KWANI ULIBEBA JUKUMU KUBWA KULIKO MTU MWINGINE YEYOTE BABA KIASI AMBACHO KILA NIKIKAA HUWA NAJIULIZA NTAKULIPA VIPI. SIWEZI KUAHIDI CHOCHOTE ILA MUNGU NDIYE ATAKAYEKULIPA. ULISIMAMA NA MIMI KILA MAHALI NA KUSIMAMISHA SHUGHULI ZAKO ZOTE KWA AJILI YANGU. NILIKURUDISHA NYUMA KWENYE KAZI ZAKO ILI TU UPATE KUNIANGALIA MIMI. ASANTE SANA BABA NA MUNGU AKUBARIKI SANA. SAMAHANI KWA KUANDIKA MENGI ILA HAPA NILIPO NI KAMA MUUJIZA TU ULIOPITA KATIKA MAISHA YANGU. ASANTE SANA MUGNU.

 




ASANTE SANA MUNGU KWANI HII YOTE NI NEEMA TU. HAPPY BIRTHDAY TO ME
NAKUPENDA SANA MAMA MAANA BILA WEWE NISINGEKUWEPO DUNIANI NA UJUE UMENIACHA KWENYE MIKONO SALAMA. R.I.P MAMA. MISS YOU

Monday 27 April 2015

NIMEIKUTA HII KWA NURU THE LIGHT, NIKAONA NIJE KU SHARE NANYI


HIVI NI VIWANGO VYA SUKARI KATIKA KILA KINYWAJI HAPO. CHAGUO NI LAKO

LATE POST, ALLIANCE ONE FAMILY DAY 2015












 
 






HAPPY BIRTHDAY LIL SIS MATTY

 
 
I want to say Happy Birthday to my cousin...sister of my heart...best friend in the world! I love you! You have always been there for me. I don't know what I would have done without you. You are my rock and I thank God everyday for you.

 
 


UNAKUMBUKA TULIKUWA TUNAFANYA SHEREHE PAMOJA?? NATAMANI HIYO HALI IJIRUDIE TENA MY DEAR. BUT ALL IN ALL HAPPY BIRTHDAY MY DEAR.

DADA LOVES YOU MUCH



 

Many years ago on this day, God decided to send an angel to earth. The angel was meant to touch lives and that happened! Happy Birthday my sweet angel.



 

Monday 13 April 2015

HII IMENIUMA KWA KWELI, POLE SANA MADAM



 ‘Ningekuwa na uwezo wa kuzaa ningekuwa nimezaa muda mrefu sana… But sina… Na siwezi kumkufuru mwenyezi mungu…. Au mngependa niwe nawaambia jinsi ninavyo hangaika usiku na mchana kupata mtoto wangu mwenyewe… Is dat wat u want…? kila ntakachofanya kwa ajili ya tumbo langu basi nitangaze… Au mnadhani siumii mnavyosema kuhusu maswala ya mtoto‘
Sentensi ya pili >>> ‘Kumbukeni na mimi pia ni binaadam… nina moyo kama nyie… au mnadhani napenda kuona wenzangu wana watoto au wana ujauzito alafu mimi sina hata wa kusingiziwa… mnaona nafurahia sio…. hivi mna nini jamani… yaani mtu unaweza weka post kwa nia nzuri then people jus come from nowea wanaanza kukuandikia maneno ya kukuumiza kabisa nafsi hadi mtu unakaa unajiuliza umemkosea nini mwenyezi Mungu‘
‘Kwani kuna niliemkosea yoyote mpaka muanze tu kunikashif na kunitolea maneno mazito namna hio… Kisa mtoto… mnadhani naipenda hii hali… hata mimi natamani kuitwa mama na hakuna kinachoniuma kama hicho…. So mnadhani sijui kama umri unaenda na maisha yenyewe sikuhizi mafupi anytime we die… Mnafikiria nisingependa kuacha hata ka copy kangu siku ndo Mungu anasema ananichukua’
‘Hata mimi natamani ningekuwa napiga picha niko na mwanangu… I want dat with all my life but I cant…. Sitokaa nimkufuru Mungu wangu hata siku moja maana sijui ni kitu gani kaniandikia… But just dont rub it in… It hurts… And im jus a human being like each and everyone of u….

YANGA AFRICA YANGA UMOJA WA MATAIFA........MALIZIA WEWEEEEE

Mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva akiwatoka Mabeki wa Timu ya Mbeya City wakati wa mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara uliochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa hivi sasa.Yanga imeishia Bao 3 - 1.

Kiungo Mchezeshaji wa timu ya Yanga, Haroun Niyonzima akiangalia kwa kupeleka mpira wakati wa mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara uliochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa hivi sasa.Yanga imeishia Bao 3 - 1.
Kipa wa Mbeya City, Hanington Kalyesubula akiangalia mpira wavuni huku washabiki wa Yanga wakishangilia ushindi wao.
Wachezaji wa timu ya Yanga wakisangilia ushindi ushindi na washabiki wao.
Picha na Othman Michuzi.