Monday 29 February 2016

TAKE IT AS IT IS!!!!!!



ILA TUMESHINDA, NDUKIIIIIIII


 Bondia Mtanzania Francis Cheka (kulia) akichapana na mpinzani wake bondia kutoka nchini Serbia, Geard Ajetovic, wakati wa pambano lao la raundi 12 la ubingwa wa Mabara , uzito wa Super Midle wa WBF lililofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye Viwanja vya Leaders Club Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Katika raundi ya kwanza bondia Cheka alionekana kuanza kwa woga na kumfanya mpinzani wake kumshambilia kwa ngumi za kushitukiza na kumpeleka chini, jambo lililomfanya Cheka kuchanganyikiwa na kuhesabiwa na mwamuzi na kisha kuendelea na pambano.

Baada ya kwenda chini katika raundi ya kwanza raundi ya pili cheka alionekana kucheza kwa tahadhari kubwa kwa kupiga na kukimbia huku mpinzani wake akionekana kujigadi muda wote na kupiga ngumi za kushitukiza zilizokuwa na madhara kwa Cheka.Katika pambano hilo Bondia Francs Cheka, aliibuka na ushindi kwa pointi.
 Cheka, alichanika katika raundi ya nane baada ya mpinzani wake kumbananisha kwenye kona iliyokuwa na utelezi ambapo aliteleza na kupoteza mwelekeo na kushambuliwa mfululizo. Na Mafoto Blog.
 Cheka akitangazwa mshindi kwa pointi na mwamuzi kutoka chama cha ngumi WBF....
 Cheka akishangilia ushindi wake.....
 Mashabiki wakimbeba cheka kwa furaha.......
 Cheka akivishwa mkanda wa ubingwa.....baada ya kutangazwa mshindi....
 Cheka akijitahidi kupangua konde la mpinzani wake....
 Cheka akijibu mapigo....
 pambano likiendelea....
 Wakiliana taimingi.....
 Mimi sijui hapa Cheka alikuwa akifanya kitu gani sijui alikuwa akikwepa konde ama akijihami kwa kutoka nduki....
 Muda wote Mserbia alionekana kujihami kwa staili hii.....
 Cheka akitupiamo ......
 Hapa sasa hata mimi sijui ilikuwa ni kitu gani kwamba ni konde zito, mieleka ama nini.....
 Cheka sijui alikuwa akifanya nini hapa....
 Mserbia akitupiamo....

 Mwamuzi akimhesabia Cheka baada ya kuanguka katika raundi ya kwanza.....
 

Thursday 25 February 2016

Mvulana wa Afghan apewa Jezi ya Messi

: BBC SWAHILI   
Image caption Mvulana wa Afghan akivalia jezi nzuri aliyotumiwa na Messi
Mvulana wa taifa la Afghanistan ambaye aligonga vichwa vya mitandao ya kijamii alipovaa fulana ya mfuko wa plastiki ilio na jina la Lionel Messi hatimaye amepata jezi nzuri kutoka kwa mshambuliaji huyo wa Argentina.
BBC ilimsaidia Messi kumtafuta mtoto huyo ambaye anajulikana kuwa shabiki mkubwa wa mchezaji huyo wa Argentina.
Murtaza Ahmadi mwenye umri wa miaka 5, anatoka katika wilaya ya Jaghori mashariki mwa mkoa wa Ghazni nchini Afghanistan.
Image caption Hii ndio jezi aliyotengeza nyumabni na kuvaa
Timu ya usimamizi wa Messi ilithibitisha siku ya Alhamisi kwamba Murtaza alitumiwa jezi ya mshambuliaji huyo wa Argentina iliotiwa saini pamoja na mpira kutoka kwa mshambuliaji huyo wa Barcelona ambaye ametuzwa kuwa mchezaji bora mara tano.
''Ninampnda Messi na fulana yangu inasema Messi ananipenda,Murtaza alisema,tayari akimuigiza mshambuliaji huyo anavyosheherekea bao lake.
Msako wa mtoto huyo katika mtandao ulisababishwa na picha moja ilioenea katika mitandao ikimuonyesha amevaa fulana ya plastiki ya Messi.
Madai baadaye yalizuka kwamba mvulana huyo ni wa Kikurdi kutoka Iraq na kwamba nyota huyo wa Barcelona alitaka kumtafuta na kumpa jezi nzuri.

SELFIE










WITH MAMA K JANNETE










HAPO CHACHA ETI KITU KIMEJIREMBA