Monday 5 August 2013

DROGBA AWATUNGUA MARA MBILI ARSENAL NA KUIPA GALATASARAY KOMBE LA EMIRATES.

 Drogba amefunga mabao dakika za lala salama Kombe la Emirates l

 Drogba akimuuza Wojciech Szczesny
  Walcott akishuhudia krosi yake ikiipa Arsenal bao la kuongoza
 Walcott akishangilia na wachezaji wenzake wa Arsenal
  Emamanuel Eboue (kulia) alikuwa Nahodha wa Galatasaray ilipomenyana na timu yake ya zamani leo, Arsenal
 Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger alivyokuwa baada ya kipigo

MSHAMBULIAJI Didier Drogba ameendelea kuwa mwiba kwa Arsenal akikumbushia enzi zake alipokuwa na jezi ya Chelsea, baada ya mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 35 leo kufunga mabao mawili na kuiwezesha klabu yake, Galatasaray kutwaa Kombe la Emirates.
Kweli, ni mashindano ya kirafiki na hayana maana yoyote katika msimu, lakini lilikuwa kama pigo lingine kwa kikosi cha Arsene Wenger.
Mfaransa huyo aliwaka ile mbaya kana kwamba mashindano hayo yana maana yoyote. Alimfokea refa wa akiba, Andre Marriner baada ya refa Jon Moss kuwazawadia penalti wapinzani dakika 12 kabla ya filimbi ya mwisho kutokana na Ignasi’s Miquel kumsukuma mshambuliaji huyo wa Ivory Coast.
Drogba alikwenda mwenyewe kupiga penalti hiyo na kumpeleka upande tofauti kipa Wojciech Szczesny na mpira alipoupiga. 
Drogba akafunga tena zikiwa zimesalia dakika nne, baada ya kupokea pasi ya Wesley Sneijder na kumuacha Per Mertesacker, kabla ya kumtungua tena Szczesny.
Arsenal ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao katika mchezo huo dakika ya 38, mfungaji Theo Walcott. 
Katika mchezo huo, kikosi cha Arsenal kilikuwa; Szczesny, Jenkinson, Sagna, Mertesacker, Gibbs/Miquel dk69, Arteta, Ramsey, Oxlade-Chamberlain, Cazorla/Zelalem dk61, Walcott na Sanogo/Giroud dk61.
Galatasaray Muslera; Semih, Riera, Chedjou, Eboue, Melo/Sarioglu dk66, Engin Baytar/Gulselam dk32,Altintop/Colak, dk45, Amrabat, Elmander/Drogba dk45, Umut Bulut/Sneijder dk45.

No comments: