Wednesday 11 September 2013

Laana: Babu mwenye watoto nane atarajia kufunga ndoa na mbuzi

Mzee mmoja anayejulikana kwa jina Aparecido Castaldo mstaafu kutoka Jundiai Brazil ameacha watu hoi kwa mshangao baada ya kutangaza nia yake ya kufunga ndoa na mbuzi wake mpenzi Carmella ambae kwa mwaka wa pili sasa anamzimia!

Babu huyo mwenye miaka 74 Aparecido ana watoto nane wanne wa kike na wanne wa kiume kutoka kwenye ndoa nne tofauti!

Anasema mbuzi ana faida na nafuu kuliko binadamu wa kawaida "Mtu anaponiona nafanya kitu kibaya au cha ajabu huwa namjibu huyu ni mbuzi..haongei,haombi hela kwa ajili ya shopping na hapati mimba pia" amesema babu huyo.

Kwa sababu hakuna kiongozi yoyote wa dini atayekubali kushiriki katika ndoa hiyo,wawili hao watafunga ndoa katika kanisa linaloabudu dini ya kishetani au unaweza kuita Igreja do Diabo october 13 huko katika mji wa Jundiai Brazil.
 Mbuzi huyo Carmelita alikula gauni lake la harusi alilonunuliwa mara ya kwanza lakini mume wake mtarajiwa amenunua lingine.
Source:mamuafrica.blogspot

No comments: