Tuesday 29 April 2014

HII NIMEIKUTA KWA SHEKIDELE, IMENITISHA KIDOGO



MA BIBI NA MABWANA AFYA MANISPAA YA MORO MPO AU?

 Kachumbari ya Chips akiliwa na nzi wa kijani wanaopenda kukaa  Chooni


Muhudumu wa banda hilo la Chipsi akimenya viazi baada ya kumaliza kuanda Kachumbali hiyo ya Chipsi.
Na Dustan Shekidele,Morogoro.
BAADHI ya wananchi wa Manispaa ya Morogoro juzi walitia timu  kwenye ofisi za Mtandao huu na kutoa dukuduku lao la  kuwataka Mabibi na
Mabwana Afya wa Manispaa ya Morogoro kutoka ofisi na kuzunguka kwenye mabanda ya Chipsi na  Mama Ntilie amabayo yanatishia Afya zao kufuatia baadhi ya mabanda hayo kukidhiri kwa uchafujambo linalotishia Afya zao.

Baada ya kupokea malalamiko hayo Mtandao huu  ulifanya uchunguzi wa kina na kubaini baadhi ya mabanda hayo kukidhiri kwa uchafu.

 Leo Shushu wa Mtadano huu alizama kinyemela ndani ya banda  moja la Chipsi na kujionea hali halisi ambapo licha ya mafuta ya kukangia chipsi kutumika zaidi ya sikutatu bila kubadilishwa kwa lengo la kupata faida kubwa.
 Balaa  liko kwenye kachumbali' ambapo mbali na baadhi ya wamiliki wa mabanda hayo kununu nyanya zilizooza'Masalo' kwa lengo la kutengenezea kachumba mwandishi wetu alishuhudia kundi kubwa la nzi wa Chooni likizajza kwenye ndoo iliyojaa kachumbani hiyo jambo ambalo ni hatari kwa Afya ya binadamu

No comments: