Thursday 25 February 2016

Mvulana wa Afghan apewa Jezi ya Messi

: BBC SWAHILI   
Image caption Mvulana wa Afghan akivalia jezi nzuri aliyotumiwa na Messi
Mvulana wa taifa la Afghanistan ambaye aligonga vichwa vya mitandao ya kijamii alipovaa fulana ya mfuko wa plastiki ilio na jina la Lionel Messi hatimaye amepata jezi nzuri kutoka kwa mshambuliaji huyo wa Argentina.
BBC ilimsaidia Messi kumtafuta mtoto huyo ambaye anajulikana kuwa shabiki mkubwa wa mchezaji huyo wa Argentina.
Murtaza Ahmadi mwenye umri wa miaka 5, anatoka katika wilaya ya Jaghori mashariki mwa mkoa wa Ghazni nchini Afghanistan.
Image caption Hii ndio jezi aliyotengeza nyumabni na kuvaa
Timu ya usimamizi wa Messi ilithibitisha siku ya Alhamisi kwamba Murtaza alitumiwa jezi ya mshambuliaji huyo wa Argentina iliotiwa saini pamoja na mpira kutoka kwa mshambuliaji huyo wa Barcelona ambaye ametuzwa kuwa mchezaji bora mara tano.
''Ninampnda Messi na fulana yangu inasema Messi ananipenda,Murtaza alisema,tayari akimuigiza mshambuliaji huyo anavyosheherekea bao lake.
Msako wa mtoto huyo katika mtandao ulisababishwa na picha moja ilioenea katika mitandao ikimuonyesha amevaa fulana ya plastiki ya Messi.
Madai baadaye yalizuka kwamba mvulana huyo ni wa Kikurdi kutoka Iraq na kwamba nyota huyo wa Barcelona alitaka kumtafuta na kumpa jezi nzuri.

No comments: