Tuesday 16 July 2013

UNAWEZA USHABIKI WEWE?? MUONE MWENZIO


Shabiki aliyejichora mgongoni tatuu ya mshambuliaji Didier Drogba ameamua kuingia uwanjani na kumuonyesha.

Shabiki huyo aliingia wakati Drogba na wachezaji wenzake wa Galatasaray walipokuwa wakipasha katika mechi kabla ya mechi ya kirafiki waliyoshinda kwa mabao 3-0 dhidi ya Shrewsbury.



Shabiki huyo alimuonyesha Drogba tatuu hiyo aliyojichora mgongoni naye akampokea vizuri, akamkumbatia na kumshukuru kasha akamuoba atoke uwanjani taratibu.


Kabla ya hapo, mashabiki wengi wa Chelsea walijitokeza kumlaki Drogba wakionyesha yeye ni nyota wa klabu hiyo ya England.

No comments: